Tuesday 8 May 2012

Mfumo shirikishi (Participatory mode) no 1

Ktk makala iliyopita tulizungumzia mifumo ya uchumi wa kiIslam kua ni mfumo shirikishi (participatory), mfumo usiokua shirikishi (non- participatory) na mfumo upitishaji (Accessory). Vilevile tulieleza kwamba mfumo shirikishi unahusika na sehemu mbili ktk biashara ambazo ni mudarabaha na musharaka (partnership), ktk makala hii tutaelezea musharaka kwa ufafanuzi zaidi.

Ushirika (partnership)

Sheria ya kiIslam imejaa aina mbalimbali za biashara, uwekezaji na mengineyo ambayo yanaweza yakamuingizia mtu faida ktk mtaji wake au ujuzi alionao. Moja ktk biashara na ambazo zilijulikana mapema kabisa ktk uIslam, ni kitu kinachojulikana kama (shirkah) ambayo kwa lugha ya kibiashara ktk wakati tulionao inajulikana kama ushirika (partnership).

Ushirika maana yake ni pale watu wawili au zaidi ya wawili watakaposhirikiana ktk biashara halali kwa kuchanganya mitaji yao (capital), juhudi au ujuzi (labour) au gharama (credit worthness) na wakawa na haki na majukumu ktk ushirikiano huo. Wakifanya hivyo watashirikiana faida au maslahi yaliyopo ktk biashara hiyo kulingana na mapatano yao kama ambavyo watashirikiana hasara kulingana na kiasi cha kila mmoja alivyoshirika ktk mtaji. Ni muhimu kukumbushana kwamba faida ya washirika inaweza kukadiriwa kwa asilimia kama vile 30% lakin faida yenyewe haiwezi kujulikana ni kiasi gani mpaka itakapopatikana. Moja ktk vitu muhimu vya kukumbushana ni kwamba ni lazima makubaliano ya kugawana faida yafanyike mwanzo kabla ya kufanyika chochote na kusiwe na uhakika (guarantee) wa kiwango cha faida (rate of return), vinginevyo ushirikiano huo utakua ni batili. Kiwango hicho cha faida kinaweza kubadilishwa wakati wowote kabla ya faida kupatikana lakin hilo haliwezi kufanyika kama faida tayari imeshaingia.

Kuna aina nyingi za ushirika ktk sheria ya kiIslam kulingana na tofauti zilizopo za kimadh habu (Islamic schools of thought) kama vile madh habu ya imam Shafii, Malik, Hanbal na Abuu Hanifa. Ingawaje swala la madh habu na athari zake ktk bank za kiIslam litajadiliwa baadae.

Aina za ushirika

Sheria ya kiIslam imeliangalia swala la kushirikiana ktk sura kuu mbili. Sura ya kwanza inajulikana kama ushirika ambao sio kwa ajili ya biashara (shirkah-al-milk) na sura ya pili ni ile ya kushirikiana kwa mikataba maalum (shirkah-al- aqd).

Moja ktk tabia za kushirikiana ni kwamba, kuna wakati watu wanaweza kushirikiana hata bila ya hiyari yao kama vile kuachiwa nyumba ya urithi. Makala yetu italiangalia kushirikiana kule kwa hiyari na kwa mikataba maalum.

Kushirikiana kwa hiyari na kwa mikataba maalum kunagawanyika ktk sehemu kuu mbili mudarabah na musharakah. Lakin kwa kua tunazungumzia musharakah (partnership) basi hapa tutaungalia musharaka tu.

Kuna aina karibu tatu za kushirikiana kwa mikataba maalum ambazo watu au kikundi cha watu au taasisi mbalimbali zinaweza kushirikiana.

1- kushirikiana ktk mtaji na juhudi (shirkah-al-amwal).
2- Kushirikiana ktk kazi na huduma lakin sio mtaji (sharikah-al-amal).
3- Kushirika ktk nia njema na gharama (credit worth) lakin hakuna mtaji unaotumika. hiyo inajulikana kama (shirkah-al-wujuh).

Kwa ujumla, wanaoshirikiana wanakua na haki sawa lakini sio lazima wawe na majukumu sawa. Musharakah ktk uislam unafanana sana na uschumi wa sasa hivi na kitu kinachojulikana kama (limited partnership structures and the holding for voting shares in a limited company).
Kwa kawaida wanaoshirikiana watakapotoa mitaji yao kuiingiza kwenye biashara, mali zao zote (assets) zitakua zinamilikiwa kwa pamoja kwa kiwango cha kila mmoja alivyoshiriki ktk mtaji.

Kushirikiana kwa ajili ya uwekezaji kunaweza kugawanyika kwenye sehemu kuu mbili

1- Kushirikiana kwa kudumu (permanent musharakah)
2- Kushikiana ambako sio kwa kudumu (diminishing musharakah)

Kushirikiana ambako sio kwa kudumu ni kule ambako mmoja wa washirika anaamua kuchukua kiasi cha ziada kila faida inapopatikana kwa malengo ya kutaka kutoka baadae ktk ushirika, atakapotimiza kiwango walichokubaliana basi anakua ametoka ktk ushirika na mali yote iliyobakia inakua ni ya upande uliobaki. Hii itaelezewa kwa ufasaha zaidi baadae.

Jinsi banki za kiIslam zinavyofanya musharakah

Tuchukue mfano wa musharakah ambao sio wa kudumu (diminishing musharakah). Mteja inaifuata bank kwa ajili ya kufanya ushirika wa kununua nyumba lakin mteja ana asilimia 20 tu ya thamani ya nyumba, kwahiyo bank inatoa asilimia 80 na baada ya nyumba kununuliwa inakodishwa kulingana na bei ya soko. Mteja analipa asilimia 80 ya kodi kwakua tayari ameshalipa asilimia 20 na analipa kiasi kingine cha kupunguza thamani iliyonunuliwa nyumba. Mwisho wa muda waliokubaliana kwa mfano miaka kumi, nyumba inakua ni mali ya mteja. Baada ya kumalizika muda uiokadiriwa bank itakua imerudisha pesa yake na imefaidika na kodi iliyotolewa ktk kipindi hicho. Hayo yote ni mbali na gharama nyingine zitakazotolewa na bank kama vile bima na kodi nyingine kama VAT.

Moja ktk vitu muhimu vya kukumbushana ni pamoja na kwamba kuna maoni tofauti ya madh habu (Islamic schools of thought) kuhusiana na swala zima la kugawana faida na hasara kwa wale wanaoshirikiana. Imam Malik na Shafii wanaona kwamba ili kushirikiana kuwe sahihi ni lazima kila mshirika apate faida kulingana na alivyoshiriki ktk mtaji, wakati imam Ahmad anaona kwamba faida inaweza kutofautina na kiwango akichoshiriki mtu ktk mtaji kama walioshirikiana wakiamua hivyo bila ya kulazimishwa tangia mwanzo. Imam Abu Hanifa anachukua msimamo wa kati ktk rai hizo mbili kwa kusema, kiasi cha faida kinaweza kutofautina na kile cha mtaji ktk mazingira ya kawaida, ingawaje, kama mshiriki mmoja aliweka masharti ya kwamba hatashiriki kwa kitu chochote baada ya kutoa mtaji (sleeping partner) basi kiwango chake cha faida hakiwezi kua zaidi ya kiwango cha mtaji aliotoa.

Kitu kingine muhimu cha kukumbushana ni kwamba kwa sababu ushirika ni uhusiano kati ya pande mbili tofauti ni lazima masharti yote ya kufunga mikataba yakamilike. Kwa mfano pande zinazoshiriki ktk mikataba ni lazima zinaruhusiwa kisheria kufunga mikataba, kwa mfano huwezi kufunga mkataba na mwendawazimu. Vilevile kusiwe na aina yoyote kulazimishana, kutumia udanganyifu na mengineyo. Kuna swala linalohusiana na mteja kushindwa kulipa kiwango alichopangiwa kwa sababu zozote, hayo yataadiliwa ktk makala zinazokuja.

Wasiwasi wa mteja au bank kupata hasara ktk ushirika

Kuna wasiwasi uliojitokeza kwamba ushirika una uwezekano mkubwa wa kuleta hasara kwa bank za kiIslam, hasara ambayo itawakumba hata wale walioshirikiana na bank wakiwemo wateja na hilo litawafanya wateja kuikimbia kuweka pesa zao bank kwa ajili ya uwekezaji.
Hoja hiyo imepanguliwa kama ifuatavyo. Uhakika ni kwamba kabla ya bank kufanya biashara yoyote inafanya uchunguzi kwanza kwamba biashara hiyo ina uwezo kiasi gani wa kuingiza faida (Feasibility study) na hata ktk bank zisizokua za kiIslam wanafanya hivyo kwanza na wakihisi kua biashara hii inaweza isiingize faida, wanakataa kujihusisha na biashara hiyo. Pamoja na mambo mengine bank haifanyi biashara ya ushirika peke yake, inafanya biashara nyingi kitu ambacho sirahisi kupata hasara ktk biashara zote hizo. Moja ktk maoni ni kwamba ushirika kama utafanywa ipasavyo, na hatua muhimu za kudhibiti hasara zitachukuliwa, mategemeo ya kuingiza faida ni makubwa zaidi kuliko yale yaliyopo ktk bank za riba.

Pamoja na kusema hivyo, uchumi wa kiIslam ni lazima ujiridhishe kwamba faida yoyote itakayoingia ni lazima iambatane na baadhi ya hatari (risk), hatari hiyo inaweza kupunguzwa kwa kutumia wataalam au kwa kufanya biashara tofauti tofauti ambapo moja ikipata hasara nyingine inapata faida. Lakin ni lazima tukubali kua hakuna uwezekano wa kuhakikisha kua biashara fulani haiwezi kupata hasara kabisa. kama unataka faida ni lazima ukubali uwezekano wa kupata hasara. Kama watu wakiwa na fikra hizo basi uwezekano wa kutokea tatizo kama ikipatikana hasara ni mdogo sana. Moja kati ya matatizo ya watu kutaka faida tu bila kukubali hasara ni tatizo linalotokana na mfumo wa kuitenganisha bank na uchumi wa kawaida na kudhania kua ni vitu viwili tofauti na kwamba bank haina uhusiano wowote na hasara inayotokana na biashara, hilo limepelekea baadhi ya bank kumuahidi mteja kiwango maalum cha faida bila kujua biashara itakwendaje kitu ambacho kimeshiriki kwa kiasi kikubwa ktk matatizo ya uchumi yanayoukumba ulimwengu.
.
Kuvunja ushirika

Kwa kawaida kuvunja ushirika kunaweza kutokea iwapo walioshirikiana walipatana hivyo tangu mwanzo wa ushirika, aidha inawezekana kuvunja ushirika kama moja kati ya sababu zifuatazo itatokea.

1-Anaetaka kujitoa ktk ushirika atakapotoa taarifa ktk kipindi cha mwisho wa musharakah ktk kipindi ambacho mali zote ziko ktk mfumo wa fedha taslim (cash). Kama kutakua na asset ambazo hazipo ktk mfumo wa cash itabidi zitiwe thamani ya cash vininevyo wahusika wengine wa ushirika wanaweza kugawana asset hizo na ikiwa ni vitu ambavyo haviwezi kugawanyika kama vile mashine basi itabidi ziuzwe.

2- Kama mmoja wa washirika akifariki basi ni juu ya warithi kuendelea na ushirika au kujitoa ambapo watastahiki fungu lao kwa utaratibu tuliyoutaja juu.
3- Kama ikitokea mmoja wa washiriki hana uwezo wa kuendelea na ushirika kwa tatizo lolote kama vile ugonjwa na mengineyo.

References

Mughni Libn Qudamah (mlango wa sharikah) Vol no 14.

Rahman, H. (2005), Financing banking through musharaka principles and applicalication. Adelaide: University of Adelaide.

Usman, T. “PRINCIPLES OF SHARI’AH GOVERNING ISLAMIC INVESTMENT FUNDS” Available from http://www.kantakji.com/fiqh/Files/Finance/1001.pdf [Accessed 30/04/2012].






No comments:

Post a Comment