Saturday 24 November 2012

Uwakala (agency)

Ili kufanya maisha yawe mepesi sheria ya kiIslam imeruhusu kitu kinachoitwa wakala (agency).

Wakala maana yake ni mtu au kikundi fulani kufanya kitu fulani kwa niaba ya mtu au kikundi kingine. Wakala ni neno la kiarabu ambalo waarabu wanalitumia kwa maana hiyo hiyo kama linavyotumika katika lugha ya Kiswahili.
Katika sheria wakala maana yake ni mkataba maalum ambao mtu au kundi fulani linafunga na mtu au kundi jengine kwa kufanya kazi zake kama ambavyo angezifanya yeye mwenyewe. Kwa mfano A atakapo mwambia B ninunulie gari mbili kutoka Japan, katika mfano huu B anachukua nafasi ya A katika haki Fulani Fulani atakazopewa na A, tunasema haki Fulani Fulani kwa sababu B anatakiwa afanye yale tu atakayoruhusiwa na A.

Kutokana na mfano huo hapo juu inawezekana pia mteja wa bank akaipa bank au shirika lolote kiasi fulani cha pesa kwa ajili ya kuzizalisha kwa malipo maalum watakayokubaliana, hapa bank au hilo shirika linakua kama mzalishaji (investment manager). Banks za kiIslam zinatumia uwakala katika maeneo mengi kama vile Musharakah, Mudarabah, Salam,Istisnaa na Ijara.

Benks za kiIslam zinautumia uwakala ili kuzizalisha pesa za mteja kwa matumizi ya kila siku ya kibenk , uwakala unakua mkubwa kila mtaji wa mteja unapokua mkubwa.
Naomba pia ifahamike vizuri kua uwakala unakua kwa malipo maalum lakini pia unaweza kua bila malipo. katika makala hii tunazungumzia uwakala wenye malipo maalum. Kisheria Katika uwakala wenye malipo maalum muwakilishi (agent) anahaki ya kupokea malipo ya utangulizi mara tu baada ya kusaini mkataba wa kazi, lakini anaweza kuadhibiwa na hata kulipiswa faini pale tu itakapogundulika kua amevunja uaminif.
Ni vizuri tukakumbushan kwamba kuhitaji muwakilishi ni suala linajitokeza pale mtu anaposhindwa kutekeleza majukumu yake kwa sababu za kitaaluma, anapokua mbali na sehemu ya matukio au kwa sababu nyengine yoyote. Kazi kubwa ya muwakilishi ni kutoa huduma ipasavyo kwa masharti maalum ya yule anaemuwakilisha. Kwa upande mwengine unaposoma Quraan (43:32) utaona ya kwamba kuwakilishana ni mgawanyo wa kimajukumu kutoka kwa muumba mwenyewe ili maisha yaweze kuendelea, kwa upande mwingine ili binadamu washirikiane ktk nema. ‘It is We Who portion out [between them] their livelihood in this world [let alone the exalted rank of prophethood] and We raised some of them above others in ranks so that some may employ others in their work. But the Mercy of your Lord is better than what they amass’.

Uwakilishi katika banks zinazofuata sheria ya kiIalam inakua ni kazi ya kitaalam zaidi, kwa mfano, kazi ya kuuza, kununua, kukodi na kukodisha, kukopa na kukopesha, kushughulikia madeni, kufunga mikataba, kupokea malipo na kulipa ,kuongoza na kutetea haki za shirika kusafirisha pesa kutoka nchi kwenda nchi nyingine na kutoka mkoa kwenda mkoa mwengine na nyenginezo nyingi.

Muwakilishi wa Banks za kiIslam anaweza kua na jukumu zaidi ya moja, suala muhimu katika uwakishi ni kufahamika sifa za uwakilishi, kwa mfano, muda,malipo,kazi zenyewe na kadhalika. Kwa maana nyengine kama wakala ni wa kuuza au kununua inatakiwa iwe wazi anauza na kununua bidhaa gani?, ukubwa gani?, ubora gani? na mengine yote muhimu yanayohusu bidhaa .
Moja ktk tofauti kubwa zilizopo kati ya uwakala unaofuata sheria za kiIslam na ule ulazima wa kwamba shughuli anazowakilishwa mtendaji ni lazima ziwe halali ktk upande wa kisheria.
Kwa maelezo zaidi usisite kuwasiliana nasi. Tunatanguliza shukran.

No comments:

Post a Comment