Wednesday 29 August 2012

Salam (Non- participatory mode no 3)

Ktk mazingira ya kawaida kuna masharti yanatakiwa yakamilike ili biashara yoyote iwe halali kwa mujibu sheria ya kiislam, kwa mfano bidhaa zinazouzwa ni lazima ziwe zipo, kwa maana kama ni mazao basi yameshavunwa, sharti nyingine, muuzaji wa bidhaa ni lazima awe ni mmiliki halali wa bidhaa hizo. Biashara ya salam kidogo ni tofauti na biashara ya kawaida kwa maana kwamba ktk biashara ya Salam imeruhusiwa kisheria kuvunja baadhi ya masharti kama vile bidhaa kutokua tayari wakati wa mauziano.

Tunaweza tukajiuliza labda ni nini hasa Salam? Salam ni kulipa thamani ya bidhaa wakati bidhaa haijakua tayari na hilo linahusika sana na bidhaa za chakula na inajulikana kwa jina la kitaalamu kama ‘forward sale generally, for crops to be grown’.

Sababu hasa ya biashara kama hii ni kuwasaidia wakulima hasa wadogowadogo ili waweze kupata vitu wanavyovihitajia kama vile mbegu, mbolea, gharama za kutayarisha mashamba na kusaidia familia zao mpaka wakati wa mavuno. Hii imekuja kama badali ya kuwaepusha wakulima kuchukua mikopo yenye riba ambayo imekatazwa na ndio maana wameruhusiwa kuuza mazao yao kabla hayaja vunwa. Kwa lugha nyingine inaweza kusemwa kwamba hii ndio sababu ya msingi ya kuruhusiwa biashara kama hii.

Ni muhimu kutaja kwamba ktk jumla ya masharti muhimu ya Salam ni kujua tarehe ya kukabidhi bidhaa, taimu, aina na kiwango cha bidhaa. Kwa maana hiyo, biashara ya Salam inatakiwa ifanyike ktk vitu ambavyo vinaweza kupimika kwa vipimo maalum na kujulikana kiasi na kiwango chake, haya yote yanafanyika kwa ajili ya kuepesha ugomvi ambao unaweza kujitokeza baadae. Wanaofanya biashara ya Salam wana hiyari ya kupanga bei ya bidhaa wanavyotaka, lakin sana inakua ni bei ndogo kuliko bei ya soko. Mununuzi ni lazima atoe thamani kamili ya bidhaa kwa sababu asipofanya hivyo itakua ni kuuza deni kwa deni biashara ambayo imezuwiwa ktk sheria.

Kwa kawaida bidhaa za biashara ya Salam zinatakiwa kukabidhiwa kwa mnunuzi ktk wakati waliokubaliana, na kama ikitokea muuzaji ameshindwa kufanya hivyo bila sababu ya msingi, basi atapigwa faini na faini hiyo itapelekwa ktk mashirika ya misaada. Ispokua muuzaji wa bidhaa anaweza kuleta bidhaa kabla ya tarehe waliokubaliana kama hilo halitasababisha usumbufu kwa mnunuzi.

Benki zinazofuata sheria za kiIslam zinaweza kufaidika na bishara ya Salam lakin hazitaruhusiwa kupokea pesa kutoka kwa wateja wake, badala yake zitatakiwa zipokee bidhaa. Wakati huohuo benki hairuhusiwi kuuza bidhaa inazotegemea kuzipata ktk biashara ya Salam mpaka zitakapo kabidhiwa. Kwa upande mwingine, muuzaji wa Salam ambae sana ni benki anayo haki ya kudai dhamana au security kwa malipo ambayo ameyatoa na kama muuzajia akishindwa kufikisha bidhaa ktk wakati uliopangwa pasi na sababu ya msingi, basi mnunuzi anaruhusiwa kuchukua bidhaa kama zile sokoni kutokana na ile dhamana aliyoiweka muuzaji.

Wasomi wa kiIslam wameruhusu muuzaji na mnunuzi kupeana muda wa kufikiri (khiyr-al- shart) ambapo kila mmoja atakua na hiyari ya kuamua kwamba kweli anataka kuingia ktk mkataba. Kwa kuangalia hali halisi ya biashara ya Salam mnunuzi kwa kua anakosa nafasi ya kuona bidhaa anayotaka kuinunua (khiyar al-royat) atapewa nafasi nyingine inayojulikana kama (khiyar-al- aib) ikiwa na maana kwamba kama bidhaa alizoletewa ziko chini ya kiwango walichokubaliana, ana hiyari ya kuzikataa bidhaa hizo.

Ktk mazingira ya kawaida mnunuzi haruhusiwa kuuza bidhaa alizozinunua ktk biashara ya salam mpaka atakapo kabidhiwa bishaa ispokua anaweza kufanya kitu ambacho kinajulikana ktk sheria kama paralle salam ambapo mnunuzi anaweza kufanya mapatano ya kumuuzia bidhaa ya salam mtu mwingine wa tatu na sio Yule aliyefanya nae biashara mwanzo, kama ambavyo haitakiwa biashara hii ya pili iwe na mahusiano na biashara ile ya salam ya kwanza kwa hali yoyote. Kama yuleyule muuzaji wa kwanza atataka kununua tena bidhaa ileile aliyoiuza kwa salam, sheria haitamruhusu kufanya hivyo na kitendo hicho kitajulikana kama (a buy- back contract).

Kwa haya machache tutaishia hapa na kama kutakua na swali, maoni na ushauri wowote basi usisite kuwasiliana nasi. Shukran.

No comments:

Post a Comment