Thursday 22 November 2012

Istisna'a

Mazingira yanayotuzunguka yana athari kubwa ktk shughuli zetu za kimaisha zikiwemo biashara. Kuna wakati ambapo misingi ya kawaida ya biashara halali inabidi itekelezwe kinyume na hali ya kawaida kwakua hilo litakua na wepesi kwa mmoja wa wanaofanya biashara.

Moja ktk biashara ambazo hazionekani kufuata misingi ya kawaida lakin ni halali na zimeruhusiwa ktk sharia ya kiIslam ni Istisna’a.
Istisna’a ni biashara ambayo inafanyika kabla ya vitu vinavyouzwa kutengenezwa. Ni lazima bei ya bidhaa ifahamike wakati wa makubaliano, kwa mfano, mnunuaji anatoa order ya kitu kitakachotengenezwa kama vile kabati, au nyumba ambayo itakabidhiwa baadae. Ili biashara ya Istisna’a iwe halali, bidhaa ambayo itatengenezwa ni lazima sifa zake ziwe wazi kwa kiasi ambacho haiwezi ikasababisha mzozo, kwa mfano ktk wakati wa leo kunaweza kua na catalogy ya vitu mbali mbali ambapo mteja anachagua kitu anachokihitaji.

Ni vyema tukakumbushana kwamba haiwezi kuitwa istasna’a kama bidhaa inayotaka kununuliwa tayari imeshatengenezwa na inajulikana, kama ambavyo Istisna’a haiwezi kufanyika ktk vitu ambavyo sio vya kutengeneza kama vile wanyama na matunda.
Hakuna ulazima wowote ktk biashara ya Istisna’a kwamba muuzaji awe ni yule mtengenezaji, kwani muuzaji anaweza kuingia mikataba maalum na mtengenezaji kwa ajili ya kutengeza vitu vinavyohitajiaka na nikwamisingi hiyo ambapo benki zinazofuata sharia za kiislam zinaweza zikaingia mkataba na watengenezaji wa bidhaa na zikauza kwa mteja kwa faida, kama ambavyo benki zinaweza kufanya kazi zote mbili ima kua muuzaji au mnunuzi wa bithaa ktk biashara ya Istisna’a. benki inaweza ikamuajiri mtu au shirika kama agenti wake kwa maridhiano ya pande mbili kwa ajili ya ufuatiliaji wa bidhaa na kuziuza pindi zitakapokua tayari au benki inaweza kumuwakilisha mtengenezaji wa bidhaa kama agenti wake. Moja ktk mambo ya kuzingatia ni kwamba mapatano endapo benki au mwingine yoyote ataitumia pande nyingine kama agenti wake, hizo zitakua ni biashara mbili tofauti, ya kwanza ni ile ya Istisna'a na yapili ni yauwakala. Benki inao uwezo vilevile wa kua na mshauri ambae atafuatilia mambo yanavyokwenda na kutoa ushauri kama bidhaa zinazotengenezwa zinafikia kiwango waliokubaliana. Gharama za mshauri huyo ni makubaliano kati ya pande mbili nani ambae atazitoa.

Istisana’a inaweza kutumika ktk biashara kubwa kama vile kujenga nyumba, madaraja, viwanda, barabara, bandari, viwanja vya ndege na mengineyo.

Kwakua biashara ya Istisna’a kuna wakati inachukua muda mrefu, bei waliopatana mteja na muuzaji inaweza ikabadilishwa kama hilo litafanyika kwa maridhianio kutoka ktk pande mbili. Unafuu mwingine ni ule unaohusiana na uwezekano wa mteja ktk biashara ya Istisna’a kulipa kidogodogo lakin ktk muda maalum watakao kubaliana. Kama hilo likifanyika basi mteja anaruhusiwa kisheria kuchukua rehani ya pesa anazozitoa kidogodogo

Ni vyema tukakumbushana kwamba ruhusa ya kulipa kidogodogo ktk biashara ya Istisna’a ni ruhusa ambayo imetolewa na wasomi wa zama tulizonazo na wametumia kitu kinachokulikana ktk sharia ya kiIslam kama (Istihsan) ambayo inajulikana kwa lugha ya kiingereza kama Juristi ‘prefence’ over strict analogy.
Kwa kawaida muuzaji anatakiwa anunue vifaa vyote kwa ajili ya bidhaa walioelewana, kama ikitokea kwamba mnunuzi amenunua vifaa na muuzaji ni mtengenezaji tu, muuzaji atachukua malipo ya bidhaa atakayoitengeneza lakin biashara hiyo haitazingatiwa kua ni Istisna’a.

Biashara ya Istisna’a haiwezi kuvunjwa na upande mmoja wakati kazi imeshaanza na kuna gharama ambazo zimeshatumika. Wasomi wengi wa wakati tulionao na Islamic fiqh Academy ya Organization of the Islamic conference (OIC) wanauzingatia mkataba wa Istisna’a kama mkataba ambao ni lazima utekelezwe (binding contract) kwa masharti fulani, kwa mfano kama bidhaa zimefikia kiwango na zimekabidhiwa ktk muda walioelewana mnunuzi hana hiyari ya kuleta masharti mengine yenye malengo ya kuvunja mkataba wake. Kama ikitokea mzaji au mnunuaji ameshindwa kutekeleza ahadi yake bila sababu za msingi, atatozwa fidia ambayo itatolewa kama msaada kwa wasiojiweza au utatolewa kwenye shughuli zozote za kheri na haitarhusiwa kutumiwa na upande wowote, kwani kufanya hivyo ni kinyume na sheria. Wanachoweza kupatana na ambacho sharia inaruhusu ni kupatana kwamba kwa mfano kama mteja atazitengeneza bidhaa kwa haraka kabla ya muda waliokubaliana basi ataipwa asilimia moja ziada au kama atachelewa atapunguziwa asiilimia moja malipo, hilo linawezekana na ziada hiyo haita takiwa kupelekwa ktk mashirika ya misaada.

Kwa hayo machache kuhusu biashara ya Istisna’a ni dhana yetu kwamba yatasaidia. Usisite kuwasiliana nasi kama kuna swali lolote kuhusiana na biashara hiyo.

No comments:

Post a Comment