Tuesday 20 March 2012

Uchumi

Mwanadamu amepata tabu sana na mambo ya kiuchumi tangu kuumbwa kwake. Inaonekana uchumi hakikua ni kitu kinachojulikana maelezo yake kwa uhakika, ingawaje, uchumi ulifahamika kama swala la kumuwezesha mwanadamu kuishi na kupata mahitaji yake fulani fulani na kuweza kujiendeleza.
Kuna maoni tofauti tofauti nini hasa maana ya kujiendeleza, kuna wale wanaoona kwamba kujiendeleza maana yake ni kupiga hatua ktk mambo yanayoonekana (Materialistic), kama ni hivyo basi, malengo ya binadamu au jamii yataelekeza juhudi zake kwenye kupata mahitaji yake binafsi na ikiwezekana kujilimbikizia  utajiri mkubwa. Hali ikiwa hivyo ni dhahiri kwamba, malengo yote na huduma zote  zinakua ni  kwa ajili ya mtu kupata maslahi binafsi na watu watakua hawana malengo ya pamoja, na kama yapo basi yatapuuzwa na kila mmoja atakua na uhuru wa kuamua kitu gani ana maslahi nacho zaidi.
Lakin kama kutakua na malengo ya kibinadamu au ya kiitikadi basi malengo ya uchumi ya jamii hiyo, yatashughulikia sana usawa ktk jamii, ajira na kugawana utajiri kwa malengo ya kunyanyajua kipato cha jamii kwa ujumla. Ni muhimu kutaja kua malengo ya kiuchumi ya jamii Fulani yatategemeana na mahitaji ya jamii hiyo.
Makala zinazokuja zitaelezea kwa ufasaha zaidi maswala aina za uchumi.

No comments:

Post a Comment