Saturday 2 June 2012

mfumo shirikishi (participatory mode) no 2

Mudarabah

Baada ya kuelezea musharakah ambao ilikua ni mmoja kati ya mifumo shirikishi (participatory modes), ktk makala hii tutaelezea aina nyingine ya mfumo shirikishi ambayo ni mudarabah (co-partnership) na mfumo huu unatumiwa sana na bank za kiIslam kutokana na faida nyingi zilizopo katika mfumo huu. Wachunguzi wa mambo ya kibiashara wanadai kwamba mataifa na mashirika mbali mbali, na hata watu binafsi duniani wanafaidika sana na mfumo huu, kwa mfano nchi kama Tanzania kwa kushirikiana na bank za kiIslam inaweza ikautumia mfumo huu katika kilimo kwanza badala ya mfumo uliopo sasa kukopesha(loarn). Kwa kuliweka wazi zaidi hilo tumeona ni muhimu tuanzie kwa kumfahamisha msomaji nini maaana ya mudarabah (co-partnership).


Maana ya mudarabah (co-partnerhip)

Mudarabah ni aina maalum ya ushirika (co-partnership) kati ya watu wawili na zaidi au makundi mawili na zaidi, upande mmoja unatoa mtaji (capital) upande huu unaitwa rabbu-ul-maal (investor or financier), na upande mwengine unatoa juhudi ktk kusimamia mtaji huo na unaitwa mjasirimali(mudarib -entrepreneur- or- labour). Kwa mfano Bank itakapotoa million 20,000,000 ikampa Ahmadi kuzizalisha, katika mfano huu bank itaitwa (investor) na Ahmadi ataitwa mjasirimali (interprenuer or labour).


Kwa kawaida ktk mudarabah inakadiriwa kua mjasirimali ni mshirika ktk biashara lakini hakutoa mtaji wa aina yoyote zaidi ya juhudi, kwani akitoa mtaji biashara hiyo kitaalamu itajulikana kama musharakah ambayo imeelezewa ktk makala iliyotangulia na sio mudarabah ambayo tunailezea hapa. Kutokaana na maelezo hayo hapo juu tunaona kwamba mudarabah ni kushirikiana katika faida kati ya mtaji(capital) na uzalishaji(labour).


Ili kuongeza uzalishaji katika jamii na ufanisi katika kazi uIslam unaruhusu kwa rabbul-mal (provider or investor) kufanya biashara hiyo hiyo na watu zaidi ya mmoja, kwa mfano bank inaweza kumpa mtaji Salim na Ahmad wote wakafanya biashara hiyo hiyo kwa pamoja na watagawawana faida kulingana na makubaliano yao. Ktk sura kama hii uhusiano kati ya Ahmad na Salim utajulikana kama musharakah wakati uhusiano kati yao wote wawili na bank utajulikana kama mudarabah.


Mudarabah ni ushirika ambao unatumika sana katika nchi zilizoendelea na hasa nchi za Ulaya magharibi na USA, kwa mfano katika maduka makubwa kama Tesco, Asda na mengineyo, wamiliki wa maduka haya wanafanya murabaha na mameneja wakubwa wa maduka haya. Ingawaje, biashara zao wakati mwengine hazitimizi baadhi ya masharti ya mudarabah kama swala zima linalohusiana na hasara kama ikitokea.


Ni ukweli usiopingika kua mudarabaha ni ushirika ambao unawafaidisha wenye mali na wale wenye elimu na vipaji mbali mbali, na ushirika aina hii kwa kiasi kikubwa umekua ni sababu ya maendeleo katika nchi nyingi za kimagharibi.


Aina za mudarabah

Mudarabah unagawanyika katika sehemu kuu mbili


1-Kuna Mudarabah usionamasharti (unrestricted- mudarabah) maana yake ni pale washirika na hasa mwenye capital (investor, finencier) asipoweka masharti yoyote katika ushirika wao.


2- mudarabah wenye masharti (restricted-mudarabah) ni ule ambao rabbul-ul-mal (investor)atakapoweka masharti maalum ndani ya biashara, masharti haya yanaweza yakawa katika aina ya biashara, mahali pa biashara na kadhalika, katika ushirika wa aina hii mtoa mtaji (investor) hatakua na haki yoyote ya kudai msingi wake kama itatokea hasara yoyote isipokua tu kama mjasirimali (interprenue-labour) atakwenda kinyume na misingi ya ushirika wao.


Ni vizuri kukumbusha kua kisheria mjasirimali anayo haki ya kufanya kitu ambacho kitaleta faida zaidi ndani ya ushirika wao ingawa atatakiwa amfahamishe mtoa mtaji (investor) juu ya alichokibuni ili kujilinda kama itatokea hasara yoyote. Kama hatamfahamisha mtoa mtaji naikatokea hasara yoyote atatakiwa alipe hata kama alikua na nia njema katika biashara yao.


Mgawano wa faida

Ili mudarabah uwe sahihi ni lazima washirika waweke wazi tangia mwanzo mgawano mzima wa faida itakayopatikana kwa kiwango cha asilimia. Mambo muhimu yatakayo angaliwa katika kujadili faida nipamojana kiasi cha faida, muda wa kugawana na ,mahali, kwa mfano washirika wanaweza kukubaliana kugawa faida kila mwaka, mwezi, au kila watakaponunua na kuuza na kadhalika. Hakuna hasa masharti maalum yaliyowekwa na sharia katika ushirika cha msingi tu nikuwa masharti yasiwe kinyume na sharia, maana yake nikua masharti ya ushirika yataachiwa washirika wenyewe, kwa mfano washirika wanaweza kugawana faida sawa kwa sawa au wanaweza wakagawa tofauti, pia washirika wanaweza kukubaliana kugawana sehemu tu ya faida na nyengine ibaki waje kugawa baadae.


Ni vizuri kujua pia kua mgawano wa faida unaweza kubadilika kulingana na biashara, kwa mfano endapo watakua wanashirikiana ktk biashara zaidi ya moja, mtoa mtaji anayohaki ya kusema kua katika biashara ya madini awe na 50% ya faida, lakini katika biashara ya magari awe na 60%, pia anayohaki ya kusema kua kama utafanya biashara nje ya nchi nitataka 60% ya faida na kama unafanya ndani ya nchi nitataka 40%. Mifano hii nikutaka kumfahamisha msomaji kwamba sharia ya kiislam imewacha masharti ya ushirika yatoke kutoka katika pande zinazoshirikiana muhimu tu yasiwe ni kinyume na sharia.

Ni muhimu pia tukakumbushana kwamba kwakua ktk mudarabah kuna mgawano wa faida, basi hakuna mshahara wowote atakaostahiki mjasirimali (labour) na hii wamekubaliana madhehebu zote (Islamic schools of thought). Kuhusu gharama zinazojitokeza katikati ya uzalishaji kama vile matumizi ya kila siku ya mjasirimali, wanachuoni wengi wanaona kua gharama zitokane na mtaji wa biashara yenyewe ingawaje Imam Ahmadi amedai kua zitatoka mfukoni mwa investor lakini Abuu Hanifa anadai kua gharama zitatoka kwa mjasirimali isipokua kama atafanya biashara nje ya mji wake hapo ndio atadai gharama muhimu kama za chakula, makazi nakadhalika. Ikitokea mjasirimali ametumia gharama zake binafsi, basi zitatolewa na kurudishiwa kabla ya mgawano wa faida.


Kuvunja au kumalizika mudarbah

Mudarabah unaweza kuvujwa wakati wowote ilimradi washirika au mmoja kati ya washirika wapeane taarifa. Kama kutakua na faida yoyote wakati wa kuvunja mudarabah basi watagawana kama walivyokubaliana, na kama hakuna basi mtoa mtaji(investor) atachukua alichotoa na hapo mudarabah utakua umefika mwisho. Inaweza ikatokea kua bishara inayofanyika sio fedha taslim ni kitu kama mashine,magari nakadhalika hapo mali hizo zitauzwa kwanza ndipo washiriki watagawa kilichopatikana, kwa mfano kama mtoa mtaji ametoa kiwanda cha sabuni kiwanda hicho kinabaki kua ni mali yake na sabuni zilizopo zitauzwa ndipo wagawane faida kwa kiwango walivyokubalian.


Kama washirika wamekubaliana muda maalum wa ushirikiano wao basi muda ukifika ushirika utakua umemalizika hapo, Kwa mfano walikubaliana ushirika wao uwe wa miaka miwili basi baada ya miaka miwili ushirika utakua umemalizika bila kuhitaji maelezo yoyote, hilo linakubalika katika Madhabu(Islamic schools of thought) ya Hanbali na Hanafi ingawa limepingwa na Shafi na Maliki. Madai ya kupinga kwao ni kwamba hili litawanyima washirika uhuru kama wanataka kuvunja ushirika na hili linaweza kusababisha uzito fulani kwa washirika.


Ingawaje, inaonyesha kua kumpa mshirika uwezo wa kuvunja ushirika wakati wowote hili nalo kwa wakati tulionao ambao bishara nyingi ni za viwanda ambazo zinahitaji muda kuzizalisha litasababisha matatizo pia. Kwa mantiki hiyo, itakua ni vigumu kumpa mshirika nguvu zisizo na mipaka katika kuvunja ushirika na imependelewa kua washiriki wasubiri mpaka uzalishaji ukamilike hata kama wamewekeana muda maalumu na umeshakamilika, isipokua zikitokea hali zisizokua za kawaida ambazo ni za kuvunja sharia.


Baada ya muda waliopatana washirika kukamilika na ikatokea kua bado washirika hawa wanataka kushirikiana, basi watafunga mikataba mipya. Kwa njia nyingine ni kwamba ushirika unakwisha kwa kufa mmoja wa washirika ispokua kama wanaomrithi watapenda kuendelea na ushirika hapa yatahitajika makubaliano mapya pia. Inaweza ikajitokeza kua mfu amezikwa kutokana na mali zake au ana deni au ameusia kitu kifanyike kutoka katika mali zake kiasi hicho kitatolewa katika fungu lake na kitakachobakia kitaendele kua katika ushirika.


Ikumbukwe kwamba mtume (sws) alishirikiana na wasio waislam katika kununua, kukopa na katika mambo mengine yaliyo ruhusiwa kiislam, na hivyo hivyo waislam wanaweza kushirikiana na wasio waislam katika mambo ikiwemo biashara zilizoruhusiwa kiislam.


Ukweli ni kwamba mwenye akili ya kawaida tu hatosita kukubaliana na mfumo huu wa ushirika kutokana na faida zilizopo. Miongoni mwa faida zake ni kuunganisha vipaji mbali mbali kufanya kazi pamoja, kwa mfano mtu anaweza kumiliki mali lakini akashidwa kuzisimamia mali hizo kwasababu moja au nyengine kama vile ugonjwa, kukosa elimu, au mtoto mdogo alieachiwa mali na wazazi wake waliofariki na kadhalika, au mtu anaweza kua na ujuzi fulani labda uashi,kulima nakadhalika lakini akawa hana vyanzo vya kuanzia kazi, ili kuifanya jamii iweze kufaidika kila mmoja na mwenzie uislam uliliona hilo ndipo iliporuhusiwa kuchanganya vipaji kwa manufaa ya jamii nzima Quraan (38:24).


Kwa kumalizia tu tunakumbushana kwamba kwa sababu mudarabah ni mapatano kati ya washirika wawili ni lazima masharti ya mkataba (contract) yakamilike na mapatano yenyewe yawe ktk mambo ambayo yanaruhusiwa kisheria. Kama kutakua na kitu chochote ambacho hakiko wazi kuhusu mtaji au asilimia ya faida watakayogawana basi mudarabah utakua ni batili.






No comments:

Post a Comment