Wednesday 18 April 2012

Mifumo ya uchumi wa kiIslam no 1

Benki za kiIslam zinafanya kazi kama benki nyingine zisizokua za kiIslam, zinakubali akiba na zinatoa huduma zote za kibenk kwa kufuata misingi ya sheria ya kiIslam. Benki za kiIslam kama zilivyo benki za kawaida zinafanya biashara na zinaingiza faida ili ziendelee kuwepo na kuendesha shughuli zake. Zinafanya hivyo kwa kupokea amana (deposit) au bank inatoa mtaji kumpa mteja kwa matumaini ya kuingiza faida

Kwa hakika kinachofanyika ni kwamba bank inapokea amana (deposit) ambazo zinabadilika kua dhamana au madeni ya bank (liabilities), kwa upande mwengine amana hizo zinakua mtaji (funds) kwa upande wa wateja au kwa (management). Amana hizo zinafanyiwa biashara zenye faida, na faida inayopatikana inakua ni mtaji wa wenye akiba zao na itakayozidi inagawanywa kwa wateja kulingana na aina ya account zao. Kwa mfano kama account zao ni za uwekezaji, basi watashiriki ktk faida hiyo na kama sio za uwekezaji basi watabakiwa na mtaji wao. Faida nyingine inagawanywa kwa washiriki wengine ktk mtaji huo ambao wanajulikana kama (shareholders). Moja kati ya tofauti kubwa iliyopo kati ya bank za kiIslam na zisizokua za kiIslam ni uhakika wa kwamba kama ikipatika hasara basi inabidi igawanywe kwa wote walioshiriki kulingana na mfumo wa kiuchumi na uliotumika na aina ya account iliyofunguliwa.

Kwa ujumla tunaweza kusema kwamba bank za kiIslam zinakubali akiba kwa kutumia aina mbili za account. Ya kwanza ni account ambayo mteja anaweza kuchukua amana yake wakati wowote (on-demand deposit account) na ya pili ni account ya uwekezaji ambayo mteja anahifadhi pesa zake kwa malengo ya uwekezaji na kwa muda maalumu.

Ktk account ambayo mteja anaweza kuchukua pesa zake wakati wowote, bank hailazimiki kumpa mteja faida yoyote. Akiba ya namna hiyo kisheria, inachukua muelekeo wa kwamba mteja ameikopesha bank mkopo ambao unajulikana kama (interest- free loan) au amehifadhi,(wadia) au ameweka kama amana (trust).

Ni muhimu kukumbushana kwamba kama itakua mteja ameweka akiba yake kwa ajili ya kuhifadhi tuu au kama amana, bank haiwezi kuifanyia biashara akiba hiyo ispokua kwa ruhusa ya mteja mwenyewe, lakini bank italazimika kurudisha akiba ya mteja wa namna hiyo hata kama bank imepata hasara.

Ktk ile account ya uwekezaji bank inatakiwa itoe faida kama ikipata faida kitu ambacho kinaonekana ktk mazingira ya kawaida kama riba ambayo kwa sheria za kiIslam na sheria za dini nyingine hairuhusiwi kama tuivyoona ktk makala zilizotangulia. Labda unaweza ukajiuliza swali kwamba ni nini hasa kinachofanya faida hiyo iwe tofauti? jawabu ni kwamba, kwa hakika kinachofanya faida hiyo iwe tofauti na riba ni mifumo ambayo banki za kiislam inaitumia ktk kuizalisha akiba hiyo, mifumo ambayo inakubalika kisheria za kiislam na ambayo inajulikana kama mifumo ya uchumi wa kiislam (Islamic modes of finance).

Ktk makala zinazokuja tutaelezea kwa upana mifumo ya uchumi wa kiIslam


No comments:

Post a Comment